• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

Karibuni Mwambao

Posted on: September 5th, 2017

Mkuu wa mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga amewatahadharisha wananchi wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda (Tanganyika) kutoendesha wala kujihusisha na shughuli za kilimo na ufugaji katika maeneo yaliyotengwa kama ushoroba, misitu ya kijiji au maeneo tengefu. Tahadhari hiyo ameitoa kwenye mkutano wa hadhara katika kata za Isengule na Ikola Agosti 4, 2017 wakati alipofanya ziara ya kikazi.

Akijibu swali la mwananchi wa Isengule Bw. Magele Kisoyi aliyetaka kufafanuliwa kama Mijeti ni hifadhi au sehemu ya kuishi binadamu, Mkuu wa Mkoa wa Katavi aliwajibu wananchi kuwa hawatakiwi kurudi kuendesha shughuli za kilimo na ufugaji katika maeneo hayo kwani eneo la Mijeti lilitengwa kama msitu wa kijiji na mapito ya wanyama pori kutoka Katavi na Kigoma.

“Wakoloni hawakuwa wajinga kutenga ushoroba wa wanyama miaka ya  1950 na ninawaagiza Mkuu wa wilaya na Mkurugenzi, atakayethubutu kulima kwenye ushoroba au maeneo tengefu mazao yake yote yafyekwe na kuchukuliwa hatua za kisheria”. Alisema Muhuga.

Kijiji cha Isengule kilifanyiwa matumizi bora ya ardhi na bado kina akiba ya ardhi ya kilimo hadi miaka 50 ijayo. Muhuga aliwashangaa wananchi wa Isengule wanaolalamika kuwa hawana maeneo ya kulima wakati eneo lililotengwa kwa shughuli za kilimo bado kubwa sana na hajui kwa nini wanakimbilia Mijeti ambapo ni mbali sana kutokea katika kijiji cha Isengule. Kutoka Isengule hadi Mijeti ni zaidi ya Kilomita 25.

Matumizi bora ya ardhi yanafanywa na uongozi wa kijiji na hupanga matumizi ya ardhi kulingana na idadi ya wananchi wake katika kijiji husika, idadi ya mifugo, huduma za kijamii na kuangalia zaidi ongezeko la watu katika kijiji kwa miaka 50 ijayo. Kila kijiji kina mipaka yake, uongozi na mamlaka kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za halmashauri za vijiji.

Shida kubwa ipo kwa viongozi wa vitongoji, vijiji na watendaji wa vijiji ambao huwapokea wahamiaji haramu pasipo kufuata utaratibu wa kijiji husika. Mtu yeyote anayetaka kuhamia katika kijiji sharti aandike barua kwa uongozi wa kijiji kuomba kuhamia katika kijiji husika na akieleza shughuli anayotaka kufanya katika kijiji hicho, idadi ya mifugo aliyonayo na ukubwa wa familia yake. Baada ya barua hiyo uongozi wa kijiji utaitisha mkutano wa hadhara kujadili maombi ya watu wanaotaka kuhamia katika kijiji hicho.

Hata hivyo, Mkuu wa mkoa aliwaagiza watendaji wa vijiji kuwa na madaftari ya wenyeji wa kijiji husika na wageni. Madaftari hayo yaandikwe watu wote yaani nyumba kwa nyumba na namba zao za simu. Na mgeni lazima aandikwe kwenye daftari la wageni akionesha ametoka wapi, anaenda wapi na hapo kijijini atakaa kwa muda gani na akifanya shughuli gani na nani mwenyeji wake.

Kiongozi wa kijiji atakayekiuka utaratibu huo atachukuliwa hatua kwani ataonekana kama yeye ndiye mchochezi wa migogoro kati ya wenyeji na wageni. Utafiti unaonesha kuwa migogoro kati ya wakulima na wafugaji inasababishwa na wahamiaji haramu. Kuna watu wachache wanaowatapeli wafugaji au wakulima kuwa wao ndio wamiliki wa maeneo ya kilimo au mapori ya misitu hata mabonde ya mito na hivyo kuwaomba wawauzie maeneo hayo. Sasa wale wageni huamini kuwa wanaishi kihalali kwenye maeneo hayo waliyotapeliwa na wahuni wachache.

Kama wewe ni mgeni na unahitaji eneo la kuchungia mifugo au kuendeshea shughuli za kilimo, ni vema ukafika kwenye ofisi za kijiji husika au ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda (Tanganyika) ili kupatiwa huduma unayohitaji.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • TANGANYIKA KUENDELEA KUWEKA MIKAKATI KUBORESHA SUALA LA LISHE, WAKUU WA IDARA YA ELIMU NA WAKUU WA SHULE WAPEWA MBINU KUSIMAMIA UPATIKANAJI CHAKULA MASHULENI.

    May 13, 2025
  • WABUNGE WA KATAVI, RUKWA NA KIGOMA WATEMBELEA BANDARI YA KAREMA; WAPONGEZA UJENZI WA MELI NA BANDARI YA KISASA.

    May 12, 2025
  • JIMBO LA UCHAGUZI LA MPANDA VIJIJINI LABADILISHWA JINA.

    May 12, 2025
  • KIKAO CHA KUPANDISHA VYEO H/W YA TANGANYIKA CHAFANYIKA

    May 08, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.