• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

RC apongeza uanzishwaji wa mnada wa saba saba Tanganyika

Posted on: July 7th, 2017

Kabungu. Mkuu wa mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda Bw. Romuli Rojas John kwa kuanzisha mnada mkubwa wa sabasaba. Pongezi hizo zimetolewa Julai 7, 2017 wakati wa uzinduzi wa mnada huo wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda.

“Mkurugenzi, umebuni kitu kizuri sana kwa Mkoa wa Katavi. Watu walikuwa hawana sehemu ya kwenda kula nyama choma na kupumzika na watoto wao siku za Jumamosi. Pia eneo hili litakuwa linatumika wakati wa maonesho ya saba saba ya Mkoa wa Katavi”. Alisema Meja Jenerali Mstaafu Muhuga.

Mkoa wa Katavi ulikuwa hauna viwanja vya maonesho ya wafanya biashara ya kila mwaka (Saba saba) sasa ni matumaini kuwa maonesho yatakuwa yanafanyikia katika viwanja hivi kila mwaka. Mnada huu utakuwa unafanyika kila Jumamosi ya wiki na siku zinaweza kuongezwa kutegemeana na uhitaji wa wafanya biashara.

Eneo la mnada lina ukubwa wa Hekari 14 na maeneo yametengwa kutegemeana na aina ya biashara. Kuna eneo lililotengwa kwa ajili ya mifugo, nyama choma, vinywaji na michezo ya watoto. Maeneo mengine ni kwa ajili ya biashara za mitumba, vyombo vya ndani, migahawa na mazao ya chakula. Kuna maeneo ya maegesho ya magari makubwa na madogo, sehemu ya kupumzikia na huduma mbali mbali.

Mnada huu utaiweka wilaya ya Tanganyika katika ramani ya Dunia kwani watalii watakao fika Mkoani Katavi watalazimika kufika kupata huduma mbali mbali katika viwanja hivyo vya Saba saba. Wananchi nao wataongeza kipato kutokana na kuuza bidhaa mbali mbali na mzunguko wa fedha utaongezeka sana.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda Bw.John amesema ataendelea kuutangaza ndani na nje ya Tanzania. Lengo ni kuhakikisha kila mfanya biashara katika mnada wa saba saba apate wateja wa kutosha.

“Nitahakikisha matamasha makubwa,  ngoma za asili na michezo mbali mbali inafanyikia katika viwanja hivi vya saba saba”.  Alisema Bw.John

Mnada uliozinduliwa unapatikana katika kijiji cha Kabungu, kitongozi cha Shongo tupendane mbele kidogo ya kiwanda cha kokoto mkono wa kushoto kama umetokea Mpanda mjini kuelekea Kigoma. Mnada wa saba saba unafikika kiurahisi kwani kuna barabara ya lami na umeme wa uhakika.Kwa wale mliowahi kufika mnada wa Dodoma au Arusha kwa Mrombo, mtagundua kuwa mnada wa saba saba ulipo Tanganyika ni zaidi ya minada yote ya Tanzania.

Ni mnada wa mazingira ya asili, misitu ya asili na unapata nyama choma iliyoandaliwa na watalaam waliobobea katika tasnia hiyo.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • TANGANYIKA KUENDELEA KUWEKA MIKAKATI KUBORESHA SUALA LA LISHE, WAKUU WA IDARA YA ELIMU NA WAKUU WA SHULE WAPEWA MBINU KUSIMAMIA UPATIKANAJI CHAKULA MASHULENI.

    May 13, 2025
  • WABUNGE WA KATAVI, RUKWA NA KIGOMA WATEMBELEA BANDARI YA KAREMA; WAPONGEZA UJENZI WA MELI NA BANDARI YA KISASA.

    May 12, 2025
  • JIMBO LA UCHAGUZI LA MPANDA VIJIJINI LABADILISHWA JINA.

    May 12, 2025
  • KIKAO CHA KUPANDISHA VYEO H/W YA TANGANYIKA CHAFANYIKA

    May 08, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.