MKUU WA MKOA KATAVI AZINDUA UPANDAJI MITI-MWESE
Mkuu wa mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga amewaongoza wananchi wa kata ya Mwese katika kuhamasisha upandaji wa miti mkoani Katavi ambapo zaidi ya miti 200 imepandwa katika eneo la kanisa. Zoezi hilo limefanyika Disemea 7, 2017katika kata ya Mwese wilayani Tanganyika .
Wananchi wa Mwese wameitikia kwa wingi na zaidi ya miti 500,000 aina ya misindano (pinus patula) inatarajiwa kugawiwa bure kwa wananchi na taasisi mbali mbali kwa lengo la kupandwa na baadaye ije kuwanufaisha watu mbali mbali. Miti hiyo imefadhiliwa na shirika la kimataifa (THE NATURE CONSERVANCY) kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Mpanda.
Licha ya The Nature Conservancy kufadhili shughuli za ua